Guru Granth Sahib Translation Project

Guru Granth Sahib Swahili Page 293

Page 293

ਨਾਨਕ ਹਰਿ ਪ੍ਰਭਿ ਆਪਹਿ ਮੇਲੇ ॥੪॥ naanak har parabh aapeh maylay. ||4|| Ee Nanak, Mungu Mwenyewe amewaunganisha naye Mwenyewe.
ਸਾਧਸੰਗਿ ਮਿਲਿ ਕਰਹੁ ਅਨੰਦ ॥ saaDh sang mil karahu anand. Jiunge na Uandamano wa Watakatifu, na ufurahie raha tele ya kweli.
ਗੁਨ ਗਾਵਹੁ ਪ੍ਰਭ ਪਰਮਾਨੰਦ ॥ gun gaavhu parabh parmaanand. Imba sifa za Mungu, udhihirisho wa raha tele kuu.
ਰਾਮ ਨਾਮ ਤਤੁ ਕਰਹੁ ਬੀਚਾਰੁ ॥ raam naam tat karahu beechaar. Tafakari kuhusu kiini cha Jina la Mungu,
ਦ੍ਰੁਲਭ ਦੇਹ ਕਾ ਕਰਹੁ ਉਧਾਰੁ ॥ darulabh dayh kaa karahu uDhaar. Na uukomboe mwili huu wa kibinadamu, ambao ni mgumu sana kuupata.
ਅੰਮ੍ਰਿਤ ਬਚਨ ਹਰਿ ਕੇ ਗੁਨ ਗਾਉ ॥ amrit bachan har kay gun gaa-o. Kariri kwa heshima nyimbo za ambrosia za Sifa za Mungu;
ਪ੍ਰਾਨ ਤਰਨ ਕਾ ਇਹੈ ਸੁਆਉ ॥ paraan taran kaa ihai su-aa-o. Hii ndiyo njia ya pekee ya kuokoa maisha yako kutokana na dhambi.
ਆਠ ਪਹਰ ਪ੍ਰਭ ਪੇਖਹੁ ਨੇਰਾ ॥ aath pahar parabh paykhahu nayraa. Hisi uwepo wa Mungu ndani mwako, saa ishirini na nne kwa siku.
ਮਿਟੈ ਅਗਿਆਨੁ ਬਿਨਸੈ ਅੰਧੇਰਾ ॥ mitai agi-aan binsai anDhayraa. Ujinga wako utaondoka, na giza ya Maya itaondolewa.
ਸੁਨਿ ਉਪਦੇਸੁ ਹਿਰਦੈ ਬਸਾਵਹੁ ॥ sun updays hirdai basaavhu. Sikiliza mafundisho ya Guru na uyathamini moyoni mwako,
ਮਨ ਇਛੇ ਨਾਨਕ ਫਲ ਪਾਵਹੁ ॥੫॥ man ichhay nanak fal paavhu. ||5|| Ee Nanak, hamu zako zote zitatimizwa.
ਹਲਤੁ ਪਲਤੁ ਦੁਇ ਲੇਹੁ ਸਵਾਰਿ ॥ halat palat du-ay layho savaar. Ipambe dunia hii na pia itakayofuata,
ਰਾਮ ਨਾਮੁ ਅੰਤਰਿ ਉਰਿ ਧਾਰਿ ॥ raam naam antar ur Dhaar. Kwa kuliweka Jina la Mungu ndani ya moyo wako.
ਪੂਰੇ ਗੁਰ ਕੀ ਪੂਰੀ ਦੀਖਿਆ ॥ pooray gur kee pooree deekhi-aa. Funzo la Guru mkamilifu ni kamili.
ਜਿਸੁ ਮਨਿ ਬਸੈ ਤਿਸੁ ਸਾਚੁ ਪਰੀਖਿਆ ॥ jis man basai tis saach pareekhi-aa. Mtu ambaye linaishi moyoni mwake, hugundua Mungu wa milele.
ਮਨਿ ਤਨਿ ਨਾਮੁ ਜਪਹੁ ਲਿਵ ਲਾਇ ॥ man tan naam japahu liv laa-ay. Kwa akili na mwili wako, kariri Naam kwa upendo na ujimakinishe kwake.
ਦੂਖੁ ਦਰਦੁ ਮਨ ਤੇ ਭਉ ਜਾਇ ॥ dookh darad man tay bha-o jaa-ay. Huzuni, uchungu na hofu itakuondoka akilini.
ਸਚੁ ਵਾਪਾਰੁ ਕਰਹੁ ਵਾਪਾਰੀ ॥ sach vaapaar karahu vaapaaree. Ee binadamu, fanya biashara ya kweli ya kutafakari kuhusu Jina la Mungu,
ਦਰਗਹ ਨਿਬਹੈ ਖੇਪ ਤੁਮਾਰੀ ॥ dargeh nibhai khayp tumaaree. Ili bidhaa (utajiri wa Naam) iidhinishwe taratibu katika mahakama ya Mungu.
ਏਕਾ ਟੇਕ ਰਖਹੁ ਮਨ ਮਾਹਿ ॥ aykaa tayk rakhahu man maahi. Weka akilini, tegemeo la kweli kwa Mungu,
ਨਾਨਕ ਬਹੁਰਿ ਨ ਆਵਹਿ ਜਾਹਿ ॥੬॥ nanak bahur na aavahi jaahi. ||6|| Ee Nanak, utakuwa huru kutoka kwa mizunguko ya kuzaliwa na kufa.
ਤਿਸ ਤੇ ਦੂਰਿ ਕਹਾ ਕੋ ਜਾਇ ॥ tis tay door kahaa ko jaa-ay. Mtu anaweza kuenda wapi, kumhepa Yeye?
ਉਬਰੈ ਰਾਖਨਹਾਰੁ ਧਿਆਇ ॥ ubrai raakhanhaar Dhi-aa-ay. Mtu anaokolewa tu kwa kutafakari kuhusu Mlinzi Mungu.
ਨਿਰਭਉ ਜਪੈ ਸਗਲ ਭਉ ਮਿਟੈ ॥ nirbha-o japai sagal bha-o mitai. Kwa kutafakari kuhusu Mungu asiye na hofu, uoga wote unaondoka,
ਪ੍ਰਭ ਕਿਰਪਾ ਤੇ ਪ੍ਰਾਣੀ ਛੁਟੈ ॥ parabh kirpaa tay paraanee chhutai. (kwa sababu) kwa Neema ya Mungu pekee, binadamu anakombolewa kutoka kwa hofu yote.
ਜਿਸੁ ਪ੍ਰਭੁ ਰਾਖੈ ਤਿਸੁ ਨਾਹੀ ਦੂਖ ॥ jis parabh raakhai tis naahee dookh. Yule ambaye analindwa na Mungu kamwe hateseki katika huzuni yoyote.
ਨਾਮੁ ਜਪਤ ਮਨਿ ਹੋਵਤ ਸੂਖ ॥ naam japat man hovat sookh. Kwa kutafakari kuhusu Naam kwa upendo na kujitolea, akili huwa yenye amani.
ਚਿੰਤਾ ਜਾਇ ਮਿਟੈ ਅਹੰਕਾਰੁ ॥ chintaa jaa-ay mitai ahaNkaar. Wasiwasi unaondoka, na ubinafsi unaangamizwa.
ਤਿਸੁ ਜਨ ਕਉ ਕੋਇ ਨ ਪਹੁਚਨਹਾਰੁ ॥ tis jan ka-o ko-ay na pahuchanhaar. Hakuna mtu anayeweza kujilinganisha na mtawa huyo wa Mungu.
ਸਿਰ ਊਪਰਿ ਠਾਢਾ ਗੁਰੁ ਸੂਰਾ ॥ sir oopar thaadhaa gur sooraa. Yule ambaye amelindwa na Mungu mwenye nguvu zote,
ਨਾਨਕ ਤਾ ਕੇ ਕਾਰਜ ਪੂਰਾ ॥੭॥ naanak taa kay kaaraj pooraa. ||7|| Ee Nanak, kazi zake zote zinatimizwa.
ਮਤਿ ਪੂਰੀ ਅੰਮ੍ਰਿਤੁ ਜਾ ਕੀ ਦ੍ਰਿਸਟਿ ॥ mat pooree amrit jaa kee darisat. Mungu, ambaye hekima yake ni kamili, na ambaye mtazamo wake ni wa ambrosia,
ਦਰਸਨੁ ਪੇਖਤ ਉਧਰਤ ਸ੍ਰਿਸਟਿ ॥ darsan paykhat uDhrat sarisat. Kwa kutazama Maono yake (kupata Fadhila zake), dunia inaokolewa.
ਚਰਨ ਕਮਲ ਜਾ ਕੇ ਅਨੂਪ ॥ charan kamal jaa kay anoop. Mungu, ambaye fadhila zake ni kuu zisizo na ulinganisho,
ਸਫਲ ਦਰਸਨੁ ਸੁੰਦਰ ਹਰਿ ਰੂਪ ॥ safal darsan sundar har roop. Ni wa kupendeza Muundo wake na wa kuthawabisha ni mwono wake.
ਧੰਨੁ ਸੇਵਾ ਸੇਵਕੁ ਪਰਵਾਨੁ ॥ Dhan sayvaa sayvak parvaan. Umebarikiwa ujitoaji wake, na amekubalika mtawa huyo katika mahakama ya Mungu.
ਅੰਤਰਜਾਮੀ ਪੁਰਖੁ ਪ੍ਰਧਾਨੁ ॥ antarjaamee purakh parDhaan. Mungu, ajuaye ndani ndiye Kiumbe Mkuu aliyeinuliwa juu zaidi.
ਜਿਸੁ ਮਨਿ ਬਸੈ ਸੁ ਹੋਤ ਨਿਹਾਲੁ ॥ jis man basai so hot nihaal. Yule, ambaye Mungu anaishi akilini mwake, huwa mwenye furaha na raha tele.
ਤਾ ਕੈ ਨਿਕਟਿ ਨ ਆਵਤ ਕਾਲੁ ॥ taa kai nikat na aavat kaal. Hofu ya kifo haimkaribii.
ਅਮਰ ਭਏ ਅਮਰਾ ਪਦੁ ਪਾਇਆ ॥ amar bha-ay amraa pad paa-i-aa. Wao wamekuwa wasioweza kufa, na wamepokea hadhi ya kutoweza kufa,
ਸਾਧਸੰਗਿ ਨਾਨਕ ਹਰਿ ਧਿਆਇਆ ॥੮॥੨੨॥ saaDhsang naanak har Dhi-aa-i-aa. ||8||22|| Ee Nanak, kwa kutafakari kuhusu Mungu katika ushirika mtakatifu.
ਸਲੋਕੁ ॥ salok. Shalok:
ਗਿਆਨ ਅੰਜਨੁ ਗੁਰਿ ਦੀਆ ਅਗਿਆਨ ਅੰਧੇਰ ਬਿਨਾਸੁ ॥ gi-aan anjan gur dee-aa agi-aan anDhayr binaas. Guru anapombariki mtu na mafuta ya hekima Takatifu, giza ya ujinga wake inaondolewa.
ਹਰਿ ਕਿਰਪਾ ਤੇ ਸੰਤ ਭੇਟਿਆ ਨਾਨਕ ਮਨਿ ਪਰਗਾਸੁ ॥੧॥ har kirpaa tay sant bhayti-aa naanak man pargaas. ||1|| Ee Nanak, kwa Neema ya Mungu, mtu anapokutana na Guru wa kweli, akili yake inaangazwa kwa maarifa matakatifu
ਅਸਟਪਦੀ ॥ ashtapadee. Ashtapadee:
ਸੰਤਸੰਗਿ ਅੰਤਰਿ ਪ੍ਰਭੁ ਡੀਠਾ ॥ satsang antar parabh deethaa. Katika Ushirika mTakatifu, Yule ambaye amemgundua Mungu ndani mwake,
ਨਾਮੁ ਪ੍ਰਭੂ ਕਾ ਲਾਗਾ ਮੀਠਾ ॥ naam parabhoo kaa laagaa meethaa huanza kuabudu Jina la Mungu.
ਸਗਲ ਸਮਿਗ੍ਰੀ ਏਕਸੁ ਘਟ ਮਾਹਿ ॥ sagal samagri aykas ghat maahi. Mtu huyu huona kila kitu cha dunia kikiwemo katika Mungu Mwenyezi,
ਅਨਿਕ ਰੰਗ ਨਾਨਾ ਦ੍ਰਿਸਟਾਹਿ ॥ anik rang naanaa daristaahi. Na matukio yasiyohesabika ya rangi na miundo tofauti yakitokana naye.
ਨਉ ਨਿਧਿ ਅੰਮ੍ਰਿਤੁ ਪ੍ਰਭ ਕਾ ਨਾਮੁ ॥ na-o niDh amrit parabh kaa naam. Jina la ambrosia la Mungu ni kama hazina tisa za dunia,
ਦੇਹੀ ਮਹਿ ਇਸ ਕਾ ਬਿਸ੍ਰਾਮੁ ॥ dayhee meh is kaa bisraam. Na linaishi katika mwili wenyewe wa binadamu.
ਸੁੰਨ ਸਮਾਧਿ ਅਨਹਤ ਤਹ ਨਾਦ ॥ sunn samaaDh anhat tah naad. Katika hali ya utafakari wa kina zaidi, muziki wa mbinguni usio na mwisho unaendelea kucheza.
ਕਹਨੁ ਨ ਜਾਈ ਅਚਰਜ ਬਿਸਮਾਦ ॥ kahan na jaa-ee achraj bismaad. Raha tele ya furaha kuu nzuri kama hiyo haiwezi kuelezwa.
ਤਿਨਿ ਦੇਖਿਆ ਜਿਸੁ ਆਪਿ ਦਿਖਾਏ ॥ tin daykhi-aa jis aap dikhaa-ay. Yule ambaye Mungu Mwenyewe anaonyesha, huihisi raha tele hii.
ਨਾਨਕ ਤਿਸੁ ਜਨ ਸੋਝੀ ਪਾਏ ॥੧॥ naanak tis jan sojhee paa-ay. ||1|| Ee Nanak, Mungu hutoa uelewa huu kwa mtawa kama huyo peke yake.
ਸੋ ਅੰਤਰਿ ਸੋ ਬਾਹਰਿ ਅਨੰਤ ॥ so antar so baahar anant. Mungu asiye na mwisho yu ndani na Mungu huyo yu nje pia.
ਘਟਿ ਘਟਿ ਬਿਆਪਿ ਰਹਿਆ ਭਗਵੰਤ ॥ ghat ghat bi-aap rahi-aa bhagvant. Mungu anaenea katika kila moyo.
ਧਰਨਿ ਮਾਹਿ ਆਕਾਸ ਪਇਆਲ ॥ Dharan maahi aakaas pa-i-aal. Yeye anaenea duniani, angani na katika maeneo ya chini ya dunia.
ਸਰਬ ਲੋਕ ਪੂਰਨ ਪ੍ਰਤਿਪਾਲ ॥ sarab lok pooran partipaal. Yeye ndiye mtunzaji kamili wa dunia zote.


© 2025 SGGS ONLINE
error: Content is protected !!
Scroll to Top