Guru Granth Sahib Translation Project

Guru Granth Sahib Swahili Page 473

Page 473

ਪਉੜੀ ॥ pa-orhee. Pauree:
ਸਤਿਗੁਰੁ ਵਡਾ ਕਰਿ ਸਾਲਾਹੀਐ ਜਿਸੁ ਵਿਚਿ ਵਡੀਆ ਵਡਿਆਈਆ ॥ satgur vadaa kar salaahee-ai jis vich vadee-aa vadi-aa-ee-aa. Tunafaa kumsifu Guru wa Kweli tukimfikiria kuwa mkuu zaidi; ambaye ndani yake kuna fadhila kuu zaidi.
ਸਹਿ ਮੇਲੇ ਤਾ ਨਦਰੀ ਆਈਆ ॥ seh maylaytaa nadree aa-ee-aa. Mungu anapotufanya tukutane na Guru, basi tunakuja kuona fadhila hizi.
ਜਾ ਤਿਸੁ ਭਾਣਾ ਤਾ ਮਨਿ ਵਸਾਈਆ ॥ jaatisbhaanaataa man vasaa-ee-aa. Inapompendeza Yeye, fadhila hizi huja kuishi katika akili zetu.
ਕਰਿ ਹੁਕਮੁ ਮਸਤਕਿ ਹਥੁ ਧਰਿ ਵਿਚਹੁ ਮਾਰਿ ਕਢੀਆ ਬੁਰਿਆਈਆ ॥ kar hukam mastak hathDhar vichahu maar kadhee-aa buri-aa-ee-aa. Akiwa mwenye huruma, Guru huondoa maovu kutoka kwa akili yetu.
ਸਹਿ ਤੁਠੈ ਨਉ ਨਿਧਿ ਪਾਈਆ ॥੧੮॥ sehtuthai na-o niDh paa-ee-aa. ||18|| Mungu anapopendezwa kabisa, hazina zote za maisha zinapatwa.
ਸਲੋਕੁ ਮਃ ੧ ॥ salok mehlaa 1. Salok, Guru wa Kwanza:
ਪਹਿਲਾ ਸੁਚਾ ਆਪਿ ਹੋਇ ਸੁਚੈ ਬੈਠਾ ਆਇ ॥ pahilaa suchaa aap ho-ay suchai baithaa aa-ay. Kwanza kabisa, baada ya kuoga na kuosha mwili wake kwa makini na kuwa “safi”, (Brahmin)huja na kuketi katika (jikoni ya mwenyeji wake) “iliyotakaswa”.
ਸੁਚੇ ਅਗੈ ਰਖਿਓਨੁ ਕੋਇ ਨ ਭਿਟਿਓ ਜਾਇ ॥ suchay agai rakhi-on ko-ay nabhiti-o jaa-ay. “chakula safi”, ambacho hakuna mtu aliyekigusa mbeleni, kinawekwa mbele yake.
ਸੁਚਾ ਹੋਇ ਕੈ ਜੇਵਿਆ ਲਗਾ ਪੜਣਿ ਸਲੋਕੁ ॥ suchaa ho-ay kai jayvi-aa lagaa parhan salok. Akiwa “ametakaswa”, yeye hula chakula hiki, na kuanza kusoma mantra takatifu.
ਕੁਹਥੀ ਜਾਈ ਸਟਿਆ ਕਿਸੁ ਏਹੁ ਲਗਾ ਦੋਖੁ ॥ kuhthee jaa-ee sati-aa kis ayhu lagaadokh. Chakula hiki “safi” hutupwa mahali pachafu (tumbo), basi nani atabeba lawama ya kuchafua lishe safi kama hiyo?
ਅੰਨੁ ਦੇਵਤਾ ਪਾਣੀ ਦੇਵਤਾ ਬੈਸੰਤਰੁ ਦੇਵਤਾ ਲੂਣੁ ਪੰਜਵਾ ਪਾਇਆ ਘਿਰਤੁ ॥ ਤਾ ਹੋਆ ਪਾਕੁ ਪਵਿਤੁ ॥ anndayvtaa paaneedayvtaa baisantardayvtaa loon panjvaa paa-i-aaghirat.taa ho-aa paak pavit. (kulingana na itikadi ya Brahmin mwenyewe), nafaka ni safi, maji ni safi; moto na chumvi ni safi; wakati kitu cha tano safi, samli (siagi iliyosafishwa), kinapoongezwa, basi chakula “safi na kilichotakaswa” kinafikiriwa kuwa tayari kuliwa.
ਪਾਪੀ ਸਿਉ ਤਨੁ ਗਡਿਆ ਥੁਕਾ ਪਈਆ ਤਿਤੁ ॥ paapee si-otan gadi-aa thukaa pa-ee-aatit. Wakati chakula hiki “safi” kinapoguswa na mwili wa binadamu wenye dhambi, chakula safi kinakuwa najisi mno (kinyesi cha mtu) hivi kwamba kinanuka na kinatemewa mate.
ਜਿਤੁ ਮੁਖਿ ਨਾਮੁ ਨ ਊਚਰਹਿ ਬਿਨੁ ਨਾਵੈ ਰਸ ਖਾਹਿ ॥ jit mukh naam na oochrahi bin naavai raskhaahi. Vivyo hivyo, mdomo ambao hautamki Jina la Mungu na unakula chakula kitamu bila kumkumbuka Mungu,
ਨਾਨਕ ਏਵੈ ਜਾਣੀਐ ਤਿਤੁ ਮੁਖਿ ਥੁਕਾ ਪਾਹਿ ॥੧॥ naanak ayvai jaanee-aitit mukh thukaa paahi. || Ee Nanak, fahamu hili, kwamba mdomo (mtu) kama huo unatemewa mate (kuaibishwa mbele za Mungu).
ਮਃ ੧ ॥ mehlaa 1. Salok, Guru wa Kwanza:
ਭੰਡਿ ਜੰਮੀਐ ਭੰਡਿ ਨਿੰਮੀਐ ਭੰਡਿ ਮੰਗਣੁ ਵੀਆਹੁ ॥ bhand jammee-aibhand nimmee-aibhand mangan vee-aahu. Mwanaume anatungwa ndani mwa mwanamke na anazaliwa toka kwa mwanamke; kwa mwanamke anapata uchumba na kuolewa.
ਭੰਡਹੁ ਹੋਵੈ ਦੋਸਤੀ ਭੰਡਹੁ ਚਲੈ ਰਾਹੁ ॥ bhandahu hovaidosteebhandahu chalai raahu. Mwanamke anakuwa rafiki yake; kupitia mwanamke, vizazi vyake huja.
ਭੰਡੁ ਮੁਆ ਭੰਡੁ ਭਾਲੀਐ ਭੰਡਿ ਹੋਵੈ ਬੰਧਾਨੁ ॥ bhand mu-aabhandbhaalee-aibhand hovai banDhaan. Akifa mwanamke wake, yeye hutafuta mwanamke mwingine; ni kupitia kwa mwanamke ambapo tunapatanishwa na dunia.
ਸੋ ਕਿਉ ਮੰਦਾ ਆਖੀਐ ਜਿਤੁ ਜੰਮਹਿ ਰਾਜਾਨ ॥ so ki-o mandaa aakhee-ai jit jameh raajaan. Tunawezaje kumuita huyo (mwanamke) mwovu, ambaye ametoa uhai kwa wafalme wote (malkia, watakatifu, na watu wengine wakuu).
ਭੰਡਹੁ ਹੀ ਭੰਡੁ ਊਪਜੈ ਭੰਡੈ ਬਾਝੁ ਨ ਕੋਇ ॥ bhandahu heebhand oopjaibhandai baajh na ko-ay. (kwa kweli) ni kutoka kwa mwanamke ambapo mwanamke mwengine anazaliwa na hakuna anayezaliwa pasipo mwanamke.
ਨਾਨਕ ਭੰਡੈ ਬਾਹਰਾ ਏਕੋ ਸਚਾ ਸੋਇ ॥ naanakbhandai baahraa ayko sachaa so-ay. Ee Nanak, ni Mungu mmoja tu wa milele ambaye amekuwepo pasi (kupitia kwa chupa ya uzazi ya) mwanamke.
ਜਿਤੁ ਮੁਖਿ ਸਦਾ ਸਾਲਾਹੀਐ ਭਾਗਾ ਰਤੀ ਚਾਰਿ ॥ jit mukh sadaa salaahee-aibhaagaa ratee chaar. Wale ambao daima wanaimba sifa za Mungu, hubarikiwa na kuonekana wazuri mbele ya Mungu.
ਨਾਨਕ ਤੇ ਮੁਖ ਊਜਲੇ ਤਿਤੁ ਸਚੈ ਦਰਬਾਰਿ ॥੨॥ naanaktay mukh oojlaytit sachaidarbaar. ||2|| Ee Nanak, nyuso zao zitang’aa katika Mahakama ya Mungu wa milele.
ਪਉੜੀ ॥ pa-orhee. Pauree:
ਸਭੁ ਕੋ ਆਖੈ ਆਪਣਾ ਜਿਸੁ ਨਾਹੀ ਸੋ ਚੁਣਿ ਕਢੀਐ ॥ sabh ko aakhai aapnaa jis naahee so chun kadhee-ai. Kila mtu ana viambatisho vya kihisia duniani humu, tafuta (na unionyeshe) mmoja ambaye hana viambatisho vyovyote.
ਕੀਤਾ ਆਪੋ ਆਪਣਾ ਆਪੇ ਹੀ ਲੇਖਾ ਸੰਢੀਐ ॥ keetaa aapo aapnaa aapay hee laykhaa sandhee-ai. (Mwishowe), kila mtu hustahimili matekeo ya vitendo vyake.
ਜਾ ਰਹਣਾ ਨਾਹੀ ਐਤੁ ਜਗਿ ਤਾ ਕਾਇਤੁ ਗਾਰਬਿ ਹੰਢੀਐ ॥ jaa rahnaa naahee ait jagtaa kaa-it gaarab handhee-ai. Wakati (tukijua kwamba) hatutabaki duniani humu milele, kwa nini tujiharibu kwa kiburi?
ਮੰਦਾ ਕਿਸੈ ਨ ਆਖੀਐ ਪੜਿ ਅਖਰੁ ਏਹੋ ਬੁਝੀਐ ॥ ਮੂਰਖੈ ਨਾਲਿ ਨ ਲੁਝੀਐ ॥੧੯॥ mandaa kisai na aakhee-ai parh akhar ayho bujhee-ai, moorkhai naal na lujhee-ai. ||19|| Baada ya kusoma maneno haya (mafundisho haya), tunapaswa kujifunza (funzo hili) kwamba hatufai kumuita yeyote mbaya, na hatufai kubishana na wapumbavu.
ਸਲੋਕੁ ਮਃ ੧ ॥ salok mehlaa 1. Salok, Guru wa Kwanza:
ਨਾਨਕ ਫਿਕੈ ਬੋਲਿਐ ਤਨੁ ਮਨੁ ਫਿਕਾ ਹੋਇ ॥ naanak fikai boli-aitan man fikaa ho-ay. Ee Nanak, yule ambaye daima anazungumza kwa kiburi, huwa mwenye kiburi.
ਫਿਕੋ ਫਿਕਾ ਸਦੀਐ ਫਿਕੇ ਫਿਕੀ ਸੋਇ ॥ fiko fikaa sadee-ai fikay fikee so Yeye huitwa mwenye na wote na ndivyo huwa sifa yake.
ਫਿਕਾ ਦਰਗਹ ਸਟੀਐ ਮੁਹਿ ਥੁਕਾ ਫਿਕੇ ਪਾਇ ॥ fikaadargeh satee-ai muhi thukaa fikay paa Mwenye kiburi anafedheheshwa, naye hakubaliki katika mahakama ya Mungu.
ਫਿਕਾ ਮੂਰਖੁ ਆਖੀਐ ਪਾਣਾ ਲਹੈ ਸਜਾਇ ॥੧॥ fikaa moorakh aakhee-ai paanaa lahai sajaa-ay. ||1|| Mtu kiburi huitwa mpumbavu naye anafedheheshwa kila mahali.
ਮਃ ੧ ॥ mehlaa 1. Salok, Guru wa Kwanza:
ਅੰਦਰਹੁ ਝੂਠੇ ਪੈਜ ਬਾਹਰਿ ਦੁਨੀਆ ਅੰਦਰਿ ਫੈਲੁ ॥ andrahujhoothay paij baahardunee-aa andar fail. Katika dunia hii kuna watu wengi ambao kindani ni waongo, lakini kinje wameweza kujizolea staha yao.
ਅਠਸਠਿ ਤੀਰਥ ਜੇ ਨਾਵਹਿ ਉਤਰੈ ਨਾਹੀ ਮੈਲੁ ॥ athsath tirath jay naaveh utrai naahee mail. Hata iwapo wanaweza kuoga katika ziara sitini na nane takatifu za hija, bado uchafu wa maovu kutoka akilini mwao hauondoki.
ਜਿਨ੍ਹ੍ਹ ਪਟੁ ਅੰਦਰਿ ਬਾਹਰਿ ਗੁਦੜੁ ਤੇ ਭਲੇ ਸੰਸਾਰਿ ॥ jinH pat andar baahar gudarh taybhalay sansaar. Wale ambao wana ukarimu na wema ndani yao lakini wanaweza kuonekana wenye kiburi kinje, ndio watu wema duniani.
ਤਿਨ੍ਹ੍ਹ ਨੇਹੁ ਲਗਾ ਰਬ ਸੇਤੀ ਦੇਖਨ੍ਹ੍ਹੇ ਵੀਚਾਰਿ ॥ tinH nayhu lagaa rab sayteedaykhnHay veechaar. Wao hukumbatia upendo kwa Mungu, na kutafakari kumtazama Yeye.
ਰੰਗਿ ਹਸਹਿ ਰੰਗਿ ਰੋਵਹਿ ਚੁਪ ਭੀ ਕਰਿ ਜਾਹਿ ॥ rang haseh rang roveh chupbhee kar jaahi. Katika Upendo wa Mungu, wanacheka, na katika Upendo wa Mungu, wanalia, na pia wanakaa kimya.
ਪਰਵਾਹ ਨਾਹੀ ਕਿਸੈ ਕੇਰੀ ਬਾਝੁ ਸਚੇ ਨਾਹ ॥ parvaah naahee kisai kayree baajh sachay naah. Wao hawamtegemei yeyote mwingine, isipokuwa Bwana wao wa Kweli.
ਦਰਿ ਵਾਟ ਉਪਰਿ ਖਰਚੁ ਮੰਗਾ ਜਬੈ ਦੇਇ ਤ ਖਾਹਿ ॥ dar vaat uparkharach mangaa jabaiday-aytakhaahi. Wao huulizia Naam kama chakula cha roho yao, na akiwapa wanaishiriki.
ਦੀਬਾਨੁ ਏਕੋ ਕਲਮ ਏਕਾ ਹਮਾ ਤੁਮ੍ਹ੍ਹਾ ਮੇਲੁ ॥ deebaan ayko kalam aykaa hamaatumHaa mayl. Kuna hakimu mmoja tu na mfumo mmoja wa haki kwa kila mmoja na watu wote wenye vitendo vizuri au vibaya mwishowe hukutana katika mahakama Yake.
ਦਰਿ ਲਏ ਲੇਖਾ ਪੀੜਿ ਛੁਟੈ ਨਾਨਕਾ ਜਿਉ ਤੇਲੁ ॥੨॥ dar la-ay laykhaa peerh chhutai naankaa ji-otayl. ||2|| Ee Nanak, katika mahakama ya Mungu, akaunti ya kila mmoja inachunguzwa na watenda dhambi huadhibiwa vikali kama mbegu za mafuta zinavyopondwa katika shinikizo la mafuta.


© 2025 SGGS ONLINE
error: Content is protected !!
Scroll to Top