Page 473
ਪਉੜੀ ॥
Pauree:
ਸਤਿਗੁਰੁ ਵਡਾ ਕਰਿ ਸਾਲਾਹੀਐ ਜਿਸੁ ਵਿਚਿ ਵਡੀਆ ਵਡਿਆਈਆ ॥
Tunafaa kumsifu Guru wa Kweli tukimfikiria kuwa mkuu zaidi; ambaye ndani yake kuna fadhila kuu zaidi.
ਸਹਿ ਮੇਲੇ ਤਾ ਨਦਰੀ ਆਈਆ ॥
Mungu anapotufanya tukutane na Guru, basi tunakuja kuona fadhila hizi.
ਜਾ ਤਿਸੁ ਭਾਣਾ ਤਾ ਮਨਿ ਵਸਾਈਆ ॥
Inapompendeza Yeye, fadhila hizi huja kuishi katika akili zetu.
ਕਰਿ ਹੁਕਮੁ ਮਸਤਕਿ ਹਥੁ ਧਰਿ ਵਿਚਹੁ ਮਾਰਿ ਕਢੀਆ ਬੁਰਿਆਈਆ ॥
Akiwa mwenye huruma, Guru huondoa maovu kutoka kwa akili yetu.
ਸਹਿ ਤੁਠੈ ਨਉ ਨਿਧਿ ਪਾਈਆ ॥੧੮॥
Mungu anapopendezwa kabisa, hazina zote za maisha zinapatwa.
ਸਲੋਕੁ ਮਃ ੧ ॥
Salok, Guru wa Kwanza:
ਪਹਿਲਾ ਸੁਚਾ ਆਪਿ ਹੋਇ ਸੁਚੈ ਬੈਠਾ ਆਇ ॥
Kwanza kabisa, baada ya kuoga na kuosha mwili wake kwa makini na kuwa “safi”, (Brahmin)huja na kuketi katika (jikoni ya mwenyeji wake) “iliyotakaswa”.
ਸੁਚੇ ਅਗੈ ਰਖਿਓਨੁ ਕੋਇ ਨ ਭਿਟਿਓ ਜਾਇ ॥
“chakula safi”, ambacho hakuna mtu aliyekigusa mbeleni, kinawekwa mbele yake.
ਸੁਚਾ ਹੋਇ ਕੈ ਜੇਵਿਆ ਲਗਾ ਪੜਣਿ ਸਲੋਕੁ ॥
Akiwa “ametakaswa”, yeye hula chakula hiki, na kuanza kusoma mantra takatifu.
ਕੁਹਥੀ ਜਾਈ ਸਟਿਆ ਕਿਸੁ ਏਹੁ ਲਗਾ ਦੋਖੁ ॥
Chakula hiki “safi” hutupwa mahali pachafu (tumbo), basi nani atabeba lawama ya kuchafua lishe safi kama hiyo?
ਅੰਨੁ ਦੇਵਤਾ ਪਾਣੀ ਦੇਵਤਾ ਬੈਸੰਤਰੁ ਦੇਵਤਾ ਲੂਣੁ ਪੰਜਵਾ ਪਾਇਆ ਘਿਰਤੁ ॥ ਤਾ ਹੋਆ ਪਾਕੁ ਪਵਿਤੁ ॥
(kulingana na itikadi ya Brahmin mwenyewe), nafaka ni safi, maji ni safi; moto na chumvi ni safi; wakati kitu cha tano safi, samli (siagi iliyosafishwa), kinapoongezwa, basi chakula “safi na kilichotakaswa” kinafikiriwa kuwa tayari kuliwa.
ਪਾਪੀ ਸਿਉ ਤਨੁ ਗਡਿਆ ਥੁਕਾ ਪਈਆ ਤਿਤੁ ॥
Wakati chakula hiki “safi” kinapoguswa na mwili wa binadamu wenye dhambi, chakula safi kinakuwa najisi mno (kinyesi cha mtu) hivi kwamba kinanuka na kinatemewa mate.
ਜਿਤੁ ਮੁਖਿ ਨਾਮੁ ਨ ਊਚਰਹਿ ਬਿਨੁ ਨਾਵੈ ਰਸ ਖਾਹਿ ॥
Vivyo hivyo, mdomo ambao hautamki Jina la Mungu na unakula chakula kitamu bila kumkumbuka Mungu,
ਨਾਨਕ ਏਵੈ ਜਾਣੀਐ ਤਿਤੁ ਮੁਖਿ ਥੁਕਾ ਪਾਹਿ ॥੧॥
Ee Nanak, fahamu hili, kwamba mdomo (mtu) kama huo unatemewa mate (kuaibishwa mbele za Mungu).
ਮਃ ੧ ॥
Salok, Guru wa Kwanza:
ਭੰਡਿ ਜੰਮੀਐ ਭੰਡਿ ਨਿੰਮੀਐ ਭੰਡਿ ਮੰਗਣੁ ਵੀਆਹੁ ॥
Mwanaume anatungwa ndani mwa mwanamke na anazaliwa toka kwa mwanamke; kwa mwanamke anapata uchumba na kuolewa.
ਭੰਡਹੁ ਹੋਵੈ ਦੋਸਤੀ ਭੰਡਹੁ ਚਲੈ ਰਾਹੁ ॥
Mwanamke anakuwa rafiki yake; kupitia mwanamke, vizazi vyake huja.
ਭੰਡੁ ਮੁਆ ਭੰਡੁ ਭਾਲੀਐ ਭੰਡਿ ਹੋਵੈ ਬੰਧਾਨੁ ॥
Akifa mwanamke wake, yeye hutafuta mwanamke mwingine; ni kupitia kwa mwanamke ambapo tunapatanishwa na dunia.
ਸੋ ਕਿਉ ਮੰਦਾ ਆਖੀਐ ਜਿਤੁ ਜੰਮਹਿ ਰਾਜਾਨ ॥
Tunawezaje kumuita huyo (mwanamke) mwovu, ambaye ametoa uhai kwa wafalme wote (malkia, watakatifu, na watu wengine wakuu).
ਭੰਡਹੁ ਹੀ ਭੰਡੁ ਊਪਜੈ ਭੰਡੈ ਬਾਝੁ ਨ ਕੋਇ ॥
(kwa kweli) ni kutoka kwa mwanamke ambapo mwanamke mwengine anazaliwa na hakuna anayezaliwa pasipo mwanamke.
ਨਾਨਕ ਭੰਡੈ ਬਾਹਰਾ ਏਕੋ ਸਚਾ ਸੋਇ ॥
Ee Nanak, ni Mungu mmoja tu wa milele ambaye amekuwepo pasi (kupitia kwa chupa ya uzazi ya) mwanamke.
ਜਿਤੁ ਮੁਖਿ ਸਦਾ ਸਾਲਾਹੀਐ ਭਾਗਾ ਰਤੀ ਚਾਰਿ ॥
Wale ambao daima wanaimba sifa za Mungu, hubarikiwa na kuonekana wazuri mbele ya Mungu.
ਨਾਨਕ ਤੇ ਮੁਖ ਊਜਲੇ ਤਿਤੁ ਸਚੈ ਦਰਬਾਰਿ ॥੨॥
Ee Nanak, nyuso zao zitang’aa katika Mahakama ya Mungu wa milele.
ਪਉੜੀ ॥
Pauree:
ਸਭੁ ਕੋ ਆਖੈ ਆਪਣਾ ਜਿਸੁ ਨਾਹੀ ਸੋ ਚੁਣਿ ਕਢੀਐ ॥
Kila mtu ana viambatisho vya kihisia duniani humu, tafuta (na unionyeshe) mmoja ambaye hana viambatisho vyovyote.
ਕੀਤਾ ਆਪੋ ਆਪਣਾ ਆਪੇ ਹੀ ਲੇਖਾ ਸੰਢੀਐ ॥
(Mwishowe), kila mtu hustahimili matekeo ya vitendo vyake.
ਜਾ ਰਹਣਾ ਨਾਹੀ ਐਤੁ ਜਗਿ ਤਾ ਕਾਇਤੁ ਗਾਰਬਿ ਹੰਢੀਐ ॥
Wakati (tukijua kwamba) hatutabaki duniani humu milele, kwa nini tujiharibu kwa kiburi?
ਮੰਦਾ ਕਿਸੈ ਨ ਆਖੀਐ ਪੜਿ ਅਖਰੁ ਏਹੋ ਬੁਝੀਐ ॥ ਮੂਰਖੈ ਨਾਲਿ ਨ ਲੁਝੀਐ ॥੧੯॥
Baada ya kusoma maneno haya (mafundisho haya), tunapaswa kujifunza (funzo hili) kwamba hatufai kumuita yeyote mbaya, na hatufai kubishana na wapumbavu.
ਸਲੋਕੁ ਮਃ ੧ ॥
Salok, Guru wa Kwanza:
ਨਾਨਕ ਫਿਕੈ ਬੋਲਿਐ ਤਨੁ ਮਨੁ ਫਿਕਾ ਹੋਇ ॥
Ee Nanak, yule ambaye daima anazungumza kwa kiburi, huwa mwenye kiburi.
ਫਿਕੋ ਫਿਕਾ ਸਦੀਐ ਫਿਕੇ ਫਿਕੀ ਸੋਇ ॥
Yeye huitwa mwenye na wote na ndivyo huwa sifa yake.
ਫਿਕਾ ਦਰਗਹ ਸਟੀਐ ਮੁਹਿ ਥੁਕਾ ਫਿਕੇ ਪਾਇ ॥
Mwenye kiburi anafedheheshwa, naye hakubaliki katika mahakama ya Mungu.
ਫਿਕਾ ਮੂਰਖੁ ਆਖੀਐ ਪਾਣਾ ਲਹੈ ਸਜਾਇ ॥੧॥
Mtu kiburi huitwa mpumbavu naye anafedheheshwa kila mahali.
ਮਃ ੧ ॥
Salok, Guru wa Kwanza:
ਅੰਦਰਹੁ ਝੂਠੇ ਪੈਜ ਬਾਹਰਿ ਦੁਨੀਆ ਅੰਦਰਿ ਫੈਲੁ ॥
Katika dunia hii kuna watu wengi ambao kindani ni waongo, lakini kinje wameweza kujizolea staha yao.
ਅਠਸਠਿ ਤੀਰਥ ਜੇ ਨਾਵਹਿ ਉਤਰੈ ਨਾਹੀ ਮੈਲੁ ॥
Hata iwapo wanaweza kuoga katika ziara sitini na nane takatifu za hija, bado uchafu wa maovu kutoka akilini mwao hauondoki.
ਜਿਨ੍ਹ੍ਹ ਪਟੁ ਅੰਦਰਿ ਬਾਹਰਿ ਗੁਦੜੁ ਤੇ ਭਲੇ ਸੰਸਾਰਿ ॥
Wale ambao wana ukarimu na wema ndani yao lakini wanaweza kuonekana wenye kiburi kinje, ndio watu wema duniani.
ਤਿਨ੍ਹ੍ਹ ਨੇਹੁ ਲਗਾ ਰਬ ਸੇਤੀ ਦੇਖਨ੍ਹ੍ਹੇ ਵੀਚਾਰਿ ॥
Wao hukumbatia upendo kwa Mungu, na kutafakari kumtazama Yeye.
ਰੰਗਿ ਹਸਹਿ ਰੰਗਿ ਰੋਵਹਿ ਚੁਪ ਭੀ ਕਰਿ ਜਾਹਿ ॥
Katika Upendo wa Mungu, wanacheka, na katika Upendo wa Mungu, wanalia, na pia wanakaa kimya.
ਪਰਵਾਹ ਨਾਹੀ ਕਿਸੈ ਕੇਰੀ ਬਾਝੁ ਸਚੇ ਨਾਹ ॥
Wao hawamtegemei yeyote mwingine, isipokuwa Bwana wao wa Kweli.
ਦਰਿ ਵਾਟ ਉਪਰਿ ਖਰਚੁ ਮੰਗਾ ਜਬੈ ਦੇਇ ਤ ਖਾਹਿ ॥
Wao huulizia Naam kama chakula cha roho yao, na akiwapa wanaishiriki.
ਦੀਬਾਨੁ ਏਕੋ ਕਲਮ ਏਕਾ ਹਮਾ ਤੁਮ੍ਹ੍ਹਾ ਮੇਲੁ ॥
Kuna hakimu mmoja tu na mfumo mmoja wa haki kwa kila mmoja na watu wote wenye vitendo vizuri au vibaya mwishowe hukutana katika mahakama Yake.
ਦਰਿ ਲਏ ਲੇਖਾ ਪੀੜਿ ਛੁਟੈ ਨਾਨਕਾ ਜਿਉ ਤੇਲੁ ॥੨॥
Ee Nanak, katika mahakama ya Mungu, akaunti ya kila mmoja inachunguzwa na watenda dhambi huadhibiwa vikali kama mbegu za mafuta zinavyopondwa katika shinikizo la mafuta.