Page 467
"ਓਨੑੀ ਮੰਦੈ ਪੈਰੁ ਨ ਰਖਿਓ ਕਰਿ ਸੁਕ੍ਰਿਤੁ ਧਰਮੁ ਕਮਾਇਆ ॥
Wao hawayakaribii maovu, lakini hu tenda mema na kuishi kwa uadilifu.
"ਓਨੑੀ ਦੁਨੀਆ ਤੋੜੇ ਬੰਧਨਾ ਅੰਨੁ ਪਾਣੀ ਥੋੜਾ ਖਾਇਆ ॥
Wamejiweka huru kutoka kwa vifungo vya kidunia, na wanakula chakula na maji kwa kiasi (kinachotosha kuishi).
ਤੂੰ ਬਖਸੀਸੀ ਅਗਲਾ ਨਿਤ ਦੇਵਹਿ ਚੜਹਿ ਸਵਾਇਆ ॥
Ee Mungu, Wewe ndiye mfadhili mkuu zaidi, Wewe hutoa kila mara, zaidi na zaidi.
ਵਡਿਆਈ ਵਡਾ ਪਾਇਆ ॥੭॥
Kwa kumtukuza Yeye, wanamgundua Mungu Mkuu.
ਸਲੋਕ ਮਃ ੧ ॥
Salok, Guru wa Kwanza:
ਪੁਰਖਾਂ ਬਿਰਖਾਂ ਤੀਰਥਾਂ ਤਟਾਂ ਮੇਘਾਂ ਖੇਤਾਂਹ ॥
Ni Mungu peke yake anayejua hesabu na hali ya wanadamu wote, miti, ziara takatifu za hija, ukingo wa mito mitakatifu, mawingu na nyanja.
ਦੀਪਾਂ ਲੋਆਂ ਮੰਡਲਾਂ ਖੰਡਾਂ ਵਰਭੰਡਾਂਹ ॥
Ni Yeye tu anayejua visiwa, mabara, dunia na mifumo ya jua ambayo ipo ulimwenguni.
ਅੰਡਜ ਜੇਰਜ ਉਤਭੁਜਾਂ ਖਾਣੀ ਸੇਤਜਾਂਹ ॥
Ni Yeye tu anayejua kuhusu viumbe wanaozaliwa kwa vyanzo vinne vya uumbaji kama vile mayai, chupa cha uzazi, ardhi na jasho.
ਸੋ ਮਿਤਿ ਜਾਣੈ ਨਾਨਕਾ ਸਰਾਂ ਮੇਰਾਂ ਜੰਤਾਹ ॥
Ee Nanak, ni Mungu tu anayejua kuhusu idadi ya bahari, milima na hali ya viumbe wanaoishi ndani mwao.
ਨਾਨਕ ਜੰਤ ਉਪਾਇ ਕੈ ਸੰਮਾਲੇ ਸਭਨਾਹ ॥
Ee Nanak, akiwa muumbaji wa viumbe hao, Yeye anawathamini wote.
ਜਿਨਿ ਕਰਤੈ ਕਰਣਾ ਕੀਆ ਚਿੰਤਾ ਭਿ ਕਰਣੀ ਤਾਹ ॥
Muumba aliyeumba uumbaji, anauchunga vilevile.
ਸੋ ਕਰਤਾ ਚਿੰਤਾ ਕਰੇ ਜਿਨਿ ਉਪਾਇਆ ਜਗੁ ॥
Ndio, Muumba huyo aliyeumba dunia, anauchunga vilevile.
ਤਿਸੁ ਜੋਹਾਰੀ ਸੁਅਸਤਿ ਤਿਸੁ ਤਿਸੁ ਦੀਬਾਣੁ ਅਭਗੁ ॥
Mbele Yake nainamisha kichwa na kutoa heshima yangu, ambaye mfumo wake wa tegemeo ni wa milele.
ਨਾਨਕ ਸਚੇ ਨਾਮ ਬਿਨੁ ਕਿਆ ਟਿਕਾ ਕਿਆ ਤਗੁ ॥੧॥
Ee Nanak, bila kutafakari kwa Jina Lake, ishara zote zingine za nje za kidini kama vile Janeu (uzi mtakatifu) na Tikka (nukta kwenye paji) hazina maana.
ਮਃ ੧ ॥
Salok, Guru wa Kwanza:
ਲਖ ਨੇਕੀਆ ਚੰਗਿਆਈਆ ਲਖ ਪੁੰਨਾ ਪਰਵਾਣੁ ॥
Mtu anaweza kutenda mamilioni ya vitendo vizuri na vyema na maelfu ya vitendo vya ukarimu ambavyo vinakubalika katika jamii.
ਲਖ ਤਪ ਉਪਰਿ ਤੀਰਥਾਂ ਸਹਜ ਜੋਗ ਬੇਬਾਣ ॥
Mtu anaweza kufanya mamilioni ya toba katika ziara takatifu, na kuenda nyikani kufanya yoga katika hali ya utulivu.
ਲਖ ਸੂਰਤਣ ਸੰਗਰਾਮ ਰਣ ਮਹਿ ਛੁਟਹਿ ਪਰਾਣ ॥
Mtu anaweza kuenda kwenye uwanja wa vita na kuonyesha mamilioni ya vitendo vya ujasiri, na hata kupoteza maisha yake hapo.
ਲਖ ਸੁਰਤੀ ਲਖ ਗਿਆਨ ਧਿਆਨ ਪੜੀਅਹਿ ਪਾਠ ਪੁਰਾਣ ॥
Mtu anaweza kupata uelewa mwingi mtakatifu na hekima takatifu kwa kufanya utafakari na kusoma Vedas na Puranas,
ਜਿਨਿ ਕਰਤੈ ਕਰਣਾ ਕੀਆ ਲਿਖਿਆ ਆਵਣ ਜਾਣੁ ॥
Muumba, Ambaye ameumba uumbaji huu na ameagizia mapema wakati wa kuzaliwa na kufa kwa mtu.
ਨਾਨਕ ਮਤੀ ਮਿਥਿਆ ਕਰਮੁ ਸਚਾ ਨੀਸਾਣੁ ॥੨॥
Ee Nanak, hila hizi zote za ujanja ni za uongo na ni bure. Neema Yake tu ni muhuri au alama ya kukubalika katika mahakama Yake.
ਪਉੜੀ ॥
Pauree:
ਸਚਾ ਸਾਹਿਬੁ ਏਕੁ ਤੂੰ ਜਿਨਿ ਸਚੋ ਸਚੁ ਵਰਤਾਇਆ ॥
Ee Mungu, Wewe ndiwe Bwana wa Kweli pekee, ambaye ametoa Ukweli (uadilifu) kila mahali.
ਜਿਸੁ ਤੂੰ ਦੇਹਿ ਤਿਸੁ ਮਿਲੈ ਸਚੁ ਤਾ ਤਿਨ੍ਹ੍ਹੀ ਸਚੁ ਕਮਾਇਆ ॥
Yeye peke yake hupokea Ukweli, ambaye Wewe unampa; kisha, yeye anatenda Ukweli.
ਸਤਿਗੁਰਿ ਮਿਲਿਐ ਸਚੁ ਪਾਇਆ ਜਿਨ੍ਹ੍ਹ ਕੈ ਹਿਰਦੈ ਸਚੁ ਵਸਾਇਆ ॥
Ni kwa kukutana na kufuata mafundisho ya Guru wa Kweli ambapo watu wamegundua Ukweli. Guru anathamini Ukweli moyoni mwao.
ਮੂਰਖ ਸਚੁ ਨ ਜਾਣਨ੍ਹ੍ਹੀ ਮਨਮੁਖੀ ਜਨਮੁ ਗਵਾਇਆ ॥
Watu wapumbavu wenye hiari binafsi hawajui, Ukweli ni nini na wanaharibu maisha yao bure.
ਵਿਚਿ ਦੁਨੀਆ ਕਾਹੇ ਆਇਆ ॥੮॥
Kwa nini wamekuja hata duniani humu?
ਸਲੋਕੁ ਮਃ ੧ ॥
Salok, Guru wa Kwanza:
ਪੜਿ ਪੜਿ ਗਡੀ ਲਦੀਅਹਿ ਪੜਿ ਪੜਿ ਭਰੀਅਹਿ ਸਾਥ ॥
Hata tukisoma na kujifunza vitabu vingi na baada ya kusoma tutengeneza marundo ya vitabu.
ਪੜਿ ਪੜਿ ਬੇੜੀ ਪਾਈਐ ਪੜਿ ਪੜਿ ਗਡੀਅਹਿ ਖਾਤ ॥
Tukisoma vitabu vingi mno kwamba mashua au mashimo mengi yanaweza kujazwa navyo.
ਪੜੀਅਹਿ ਜੇਤੇ ਬਰਸ ਬਰਸ ਪੜੀਅਹਿ ਜੇਤੇ ਮਾਸ ॥
Tunaweza kuvisoma mwaka baada ya mwaka; tunaweza kuvisoma kwa miezi mingi kama ilivyo katika mwaka.
ਪੜੀਐ ਜੇਤੀ ਆਰਜਾ ਪੜੀਅਹਿ ਜੇਤੇ ਸਾਸ ॥
Tunaweza kuvisoma maisha yetu yote; tunaweza kuvisoma kwa kila pumzi.
ਨਾਨਕ ਲੇਖੈ ਇਕ ਗਲ ਹੋਰੁ ਹਉਮੈ ਝਖਣਾ ਝਾਖ ॥੧॥
Ee Nanak, kitu kimoja tu, ambacho kinahesabika katika mahakama yake ni kuimba sifa Zake na kutafakari kuhusu Jina Lake. Vyote vingine ni kama kuzurura katika ubinafsi wa mtu.
ਮਃ ੧ ॥
Salok, Guru wa Kwanza:
ਲਿਖਿ ਲਿਖਿ ਪੜਿਆ ॥ਤੇਤਾ ਕੜਿਆ ॥
Mtu anavyozidi kuandika na kusoma, ndivyo anavyozidi kuwa mwenye ubinafsi na kiburi.
ਬਹੁ ਤੀਰਥ ਭਵਿਆ ॥ਤੇਤੋ ਲਵਿਆ ॥
Mtu anavyozidi kuzurura katika ziara takatifu za hija, ndivyo anavyozidi kuzungumza bure (kama kunguru)
ਬਹੁ ਭੇਖ ਕੀਆ ਦੇਹੀ ਦੁਖੁ ਦੀਆ ॥
Mtu anavyozidi kuvaa joho la kidini, ndivyo anavyozidi kujifadhaisha.
ਸਹੁ ਵੇ ਜੀਆ ਅਪਣਾ ਕੀਆ ॥
Ee rafiki yangu, unapaswa kustahimili matokeo ya vitendo vyako mwenyewe.
ਅੰਨੁ ਨ ਖਾਇਆ ਸਾਦੁ ਗਵਾਇਆ ॥
Kwa kukosa kula chakula, mtu hajapata sifa zozote za kiroho, yeye amepoteza tu fursa ya kufurahia kiburudisho chake.
ਬਹੁ ਦੁਖੁ ਪਾਇਆ ਦੂਜਾ ਭਾਇਆ ॥
Kwa ajili ya upendo wake wa uwili (matendo balina kumpenda na kumkumbuka Mungu), yeye ameteseka Uchungu mwingi.
ਬਸਤ੍ਰ ਨ ਪਹਿਰੈ ॥ ਅਹਿਨਿਸਿ ਕਹਰੈ ॥
Yule asiyevaa mavazi yoyote, anateseka usiku na mchana kwa kutiisha mwili wake kwa makali ya hali ya anga.
ਮੋਨਿ ਵਿਗੂਤਾ ॥ ਕਿਉ ਜਾਗੈ ਗੁਰ ਬਿਨੁ ਸੂਤਾ ॥
Akizama katika kimya, mtu amepotoka (kutoka njia ya uadilifu). Anawezaje kuamshwa kutoka kwa usingizi wa ujinga bila mafundisho ya Guru?
ਪਗ ਉਪੇਤਾਣਾ ॥ ਅਪਣਾ ਕੀਆ ਕਮਾਣਾ ॥
Yule anayetembea miguumitupu, anateseka kutokana na vitendo vyake mwenyewe kwa kuumiza miguu yake.
ਅਲੁ ਮਲੁ ਖਾਈ ਸਿਰਿ ਛਾਈ ਪਾਈ ॥
Yule anayekula mabaki machafu na kurusha majivu kichwani pake,
ਮੂਰਖਿ ਅੰਧੈ ਪਤਿ ਗਵਾਈ ॥
Mtu huyo kipofu mpumbavu (mjinga) amepoteza staha yake.
ਵਿਣੁ ਨਾਵੈ ਕਿਛੁ ਥਾਇ ਨ ਪਾਈ ॥
Bila kutafakari kuhusu Jina la Mungu, hakuna kilichoidhinishwa katika mahakama Yake.
ਰਹੈ ਬੇਬਾਣੀ ਮੜੀ ਮਸਾਣੀ ॥
Mtu anaweza kuishi nyikani, makaburini au kwenye nyanja za kuchomea maiti,
ਅੰਧੁ ਨ ਜਾਣੈ ਫਿਰਿ ਪਛੁਤਾਣੀ ॥
Kipofu wa kiroho kama huyo hajui njia ya kweli ya kumgundua Mungu, yeye hujuta na kutubu mwishowe.