Page 295
ਜਿਸੁ ਪ੍ਰਸਾਦਿ ਸਭੁ ਜਗਤੁ ਤਰਾਇਆ ॥
jis parsaad sabh jagat taraa-i-aa.
Ambaye kwa neema yake, dunia nzima inaokolewa.
ਜਨ ਆਵਨ ਕਾ ਇਹੈ ਸੁਆਉ ॥
jan aavan kaa ihai su-aa-o.
Mtawa wa Mungu kama huyo anakuja duniani ili,
ਜਨ ਕੈ ਸੰਗਿ ਚਿਤਿ ਆਵੈ ਨਾਉ ॥
jan kai sang chit aavai naa-o.
Wote ambao wanakutana naye wanaanza kutafakari kuhusu Naam.
ਆਪਿ ਮੁਕਤੁ ਮੁਕਤੁ ਕਰੈ ਸੰਸਾਰੁ ॥
aap mukat mukat karai sansaar.
Mtu kama huto amekombolewa mwenyewe, na anaikomboa dunia nzima iliyosalia.
ਨਾਨਕ ਤਿਸੁ ਜਨ ਕਉ ਸਦਾ ਨਮਸਕਾਰੁ ॥੮॥੨੩॥
naanak tis jan ka-o sadaa namaskaar. ||8||23||
Ee Nanak, nasujudu kwa heshima milele kwa huyo mtawa wa Mungu.
ਸਲੋਕੁ ॥
salok.
Shalok:
ਪੂਰਾ ਪ੍ਰਭੁ ਆਰਾਧਿਆ ਪੂਰਾ ਜਾ ਕਾ ਨਾਉ ॥
pooraa parabh aaraaDhi-aa pooraa jaa kaa naa-o.
Mtu ambaye ametafakari kuhusu Mungu huyo mkamilifu ambaye Jina lake ni la milele.
ਨਾਨਕ ਪੂਰਾ ਪਾਇਆ ਪੂਰੇ ਕੇ ਗੁਨ ਗਾਉ ॥੧॥
naanak pooraa paa-i-aa pooray kay gun gaa-o. ||1||
Ee Nanak, mtu huyo amegundua Mungu mkamilifu. Hivyo basi, pia wewe unafaa kuimba sifa za yule Mmoja mkamilifu.
ਅਸਟਪਦੀ ॥
asatpadee.
Ashtapadee:
ਪੂਰੇ ਗੁਰ ਕਾ ਸੁਨਿ ਉਪਦੇਸੁ ॥
pooray gur kaa sun updays.
Ee akili yangu, sikiliza mafundisho ya Guru mkamilifu;
ਪਾਰਬ੍ਰਹਮੁ ਨਿਕਟਿ ਕਰਿ ਪੇਖੁ ॥
paarbarahm nikat kar paykh.
Na uhisi Mungu Mkuu akiwa karibu nawe.
ਸਾਸਿ ਸਾਸਿ ਸਿਮਰਹੁ ਗੋਬਿੰਦ ॥
saas saas simrahu gobind.
Tafakari kumhusu Mungu kwa kila pumzi unayopumua (kila wakati),
ਮਨ ਅੰਤਰ ਕੀ ਉਤਰੈ ਚਿੰਦ ॥
man antar kee utrai chind.
Ili wasiwasi uondoke akilini mwako.
ਆਸ ਅਨਿਤ ਤਿਆਗਹੁ ਤਰੰਗ ॥
aas anit ti-aagahu tarang.
Ee akili yangu, achana na mawimbi ya tamaa ya vitu vya mpito,
ਸੰਤ ਜਨਾ ਕੀ ਧੂਰਿ ਮਨ ਮੰਗ ॥
sant janaa kee Dhoor man mang.
Na uulizie huduma nyenyekevu ya watu watakatifu.
ਆਪੁ ਛੋਡਿ ਬੇਨਤੀ ਕਰਹੁ ॥
aap chhod bayntee karahu.
Kwa kukana majivuno yako binafsi, toa ombi nyenyekevu kwa Mungu,
ਸਾਧਸੰਗਿ ਅਗਨਿ ਸਾਗਰੁ ਤਰਹੁ ॥
saaDhsang agan saagar tarahu.
Na katika uandamano wa watu watakatifu, ogelea uivuke bahari ya moto ya dhambi.
ਹਰਿ ਧਨ ਕੇ ਭਰਿ ਲੇਹੁ ਭੰਡਾਰ ॥
har Dhan kay bhar layho bhandaar.
Jaza moyo wako na utajiri wa Jina la Mungu,
ਨਾਨਕ ਗੁਰ ਪੂਰੇ ਨਮਸਕਾਰ ॥੧॥
nanak gur pooray namaskaar. ||1||
Na Ee Nanak, sujudu kwa unyenyekevu kwa Guru Mkamilifu.
ਖੇਮ ਕੁਸਲ ਸਹਜ ਆਨੰਦ ॥
khaym kushal sahj anand.
Utabarikiwa na amani ya milele, starehe za maisha, na raha tele ya usawa.
ਸਾਧਸੰਗਿ ਭਜੁ ਪਰਮਾਨੰਦ ॥
saaDhsang bhaj parmaanand.
Kwa kutafakari kwa upendo kumhusu Mungu mkuu katika ushirika mtakatifu.
ਨਰਕ ਨਿਵਾਰਿ ਉਧਾਰਹੁ ਜੀਉ ॥
narak nivaar uDhaarahu jee-o.
Okoa moyo wako kutoka maumivu ya jehanamu,
ਗੁਨ ਗੋਬਿੰਦ ਅੰਮ੍ਰਿਤ ਰਸੁ ਪੀਉ ॥
gun gobind amrit ras pee-o.
Kwa kuimba sifa za Mungu na kwa kushiriki dawa ya Naam.
ਚਿਤਿ ਚਿਤਵਹੁ ਨਾਰਾਇਣ ਏਕ ॥
chit chitvahu naaraa-in ayk.
Tafakari kumhusu Mungu Mmoja akilini mwako,
ਏਕ ਰੂਪ ਜਾ ਕੇ ਰੰਗ ਅਨੇਕ ॥
ayk roop jaa kay rang anayk.
Ambaye ni Mmoja, lakini anayedhihirika katika miundo mingi.
ਗੋਪਾਲ ਦਾਮੋਦਰ ਦੀਨ ਦਇਆਲ ॥
gopaal daamodar deen da-i-aal.
Mtunzaji wa Ulimwengu, Bwana wa dunia na mfadhili kwa wapole,
ਦੁਖ ਭੰਜਨ ਪੂਰਨ ਕਿਰਪਾਲ ॥
dukh bhanjan pooran kirpaal.
Yeye ndiye mwangamizi wa huzuni, anayeenea kote na mwenye huruma.
ਸਿਮਰਿ ਸਿਮਰਿ ਨਾਮੁ ਬਾਰੰ ਬਾਰ ॥
simar simar naam baaraN baar.
Kwa upendo na ujitoaji kumbuka Jina lake tena na tena.
ਨਾਨਕ ਜੀਅ ਕਾ ਇਹੈ ਅਧਾਰ ॥੨॥
naanak jee-a kaa ihai aDhaar. ||2||
Ee Nanak, Naam ndiyo tegemeo pekee ya roho.
ਉਤਮ ਸਲੋਕ ਸਾਧ ਕੇ ਬਚਨ ॥
utam salok saaDh kay bachan.
Maneno ya Guru ndiyo nyimbo tukufu zaidi.
ਅਮੁਲੀਕ ਲਾਲ ਏਹਿ ਰਤਨ ॥
amuleek laal ayhi ratan.
Hayo ni kama lulu na vito visivyokadirika.
ਸੁਨਤ ਕਮਾਵਤ ਹੋਤ ਉਧਾਰ ॥
sunat kamaavat hot uDhaar.
Yule anayesikiliza na kutenda kwa haya anakombolewa kutoka kwa mizunguko ya kuzaliwa na kufa.
ਆਪਿ ਤਰੈ ਲੋਕਹ ਨਿਸਤਾਰ ॥
aap tarai lokah nistaar.
Yeye huogelea na kuvuka bahari dunia ya dhambi na anawasaidia wengine kuvuka pia.
ਸਫਲ ਜੀਵਨੁ ਸਫਲੁ ਤਾ ਕਾ ਸੰਗੁ ॥
safal jeevan safal taa kaa sang.
Maisha yake yametimizwa, na mahusiano yake ni yenye manufaa,
ਜਾ ਕੈ ਮਨਿ ਲਾਗਾ ਹਰਿ ਰੰਗੁ ॥
jaa kai man laagaa har rang.
Ambaye akili yake imejawa na upendo wa Mungu.
ਜੈ ਜੈ ਸਬਦੁ ਅਨਾਹਦੁ ਵਾਜੈ ॥
jai jai sabad anaahad vaajai.
Ndani mwake mnatetema muziki mtakatifu na mwisho unaomfanya mchangamfu sana.
ਸੁਨਿ ਸੁਨਿ ਅਨਦ ਕਰੇ ਪ੍ਰਭੁ ਗਾਜੈ ॥
sun sun anad karay parabh gaajai.
Kwa kuisikiza tena na tena yeye huwakatika raha tele anapofurahiautambuzi wa Mungu ndani mwake.
ਪ੍ਰਗਟੇ ਗੁਪਾਲ ਮਹਾਂਤ ਕੈ ਮਾਥੇ ॥
pargatay gupaal mahaaNt kai maathay.
Bwana wa ulimwengu hujidhihirisha kupitia mtu mtakatifu.
ਨਾਨਕ ਉਧਰੇ ਤਿਨ ਕੈ ਸਾਥੇ ॥੩॥
naanak uDhray tin kai saathay. ||3||
Ee Nanak, pamoja na mtu kama huyo, wengi zaidi wanakombolewa.
ਸਰਨਿ ਜੋਗੁ ਸੁਨਿ ਸਰਨੀ ਆਏ ॥
saran jog sun sarnee aa-ay.
Tuliposikia kwamba unaweza kutupa makao, tulikimbilia kwako,
ਕਰਿ ਕਿਰਪਾ ਪ੍ਰਭ ਆਪ ਮਿਲਾਏ ॥
kar kirpaa parabh aap milaa-ay.
Ee Mungu, kwa kutawaza huruma yako, Wewe umetuunganisha nawe Mwenyewe.
ਮਿਟਿ ਗਏ ਬੈਰ ਭਏ ਸਭ ਰੇਨ ॥
mit ga-ay bair bha-ay sabh rayn.
Sasa chuki yetu imeondoka na tumekuwa wanyenyekevu kabisa kwa kila mtu.
ਅੰਮ੍ਰਿਤ ਨਾਮੁ ਸਾਧਸੰਗਿ ਲੈਨ ॥
amrit naam saaDhsang lain.
Sisi tunatafakari kuhusu Naam ya ambrosia katika ushirika mtakatifu.
ਸੁਪ੍ਰਸੰਨ ਭਏ ਗੁਰਦੇਵ ॥
suparsan bha-ay gurdayv.
Guru Mtakatifu amependezwa mno;
ਪੂਰਨ ਹੋਈ ਸੇਵਕ ਕੀ ਸੇਵ ॥
pooran ho-ee sayvak kee sayv.
Na hivyo huduma ya watawa imetuzwa.
ਆਲ ਜੰਜਾਲ ਬਿਕਾਰ ਤੇ ਰਹਤੇ ॥
aal janjaal bikaar tay rahtay.
Sasa, tumeokolewa kutoka misongamano ya kidunia na dhambi,
ਰਾਮ ਨਾਮ ਸੁਨਿ ਰਸਨਾ ਕਹਤੇ ॥
raam naam sun rasnaa kahtay.
Kwa kusikiliza na kutamka Jina la Mungu,
ਕਰਿ ਪ੍ਰਸਾਦੁ ਦਇਆ ਪ੍ਰਭਿ ਧਾਰੀ ॥
kar parsaad da-i-aa parabh Dhaaree.
Kwa Neema yake, Mungu ametawaza Huruma yake,
ਨਾਨਕ ਨਿਬਹੀ ਖੇਪ ਹਮਾਰੀ ॥੪॥
naanak nibhee khayp hamaaree. ||4||
na Ee Nanak, utajiri wa Naam umekubalika katika mahakama ya Mungu.
ਪ੍ਰਭ ਕੀ ਉਸਤਤਿ ਕਰਹੁ ਸੰਤ ਮੀਤ ॥
parabh kee ustat karahu sant meet.
Enyi marafiki zangu watakatifu, imbeni sifa za Mungu,
ਸਾਵਧਾਨ ਏਕਾਗਰ ਚੀਤ ॥
saavDhaan aykaagar cheet.
Kwa umakini kamili na nia moja.
ਸੁਖਮਨੀ ਸਹਜ ਗੋਬਿੰਦ ਗੁਨ ਨਾਮ ॥
sukhmanee sahj gobind gun naam.
Sifa za Mungu na Jina la Mungu ni kito cha taji cha amani na utulivu wa mbinguni.
ਜਿਸੁ ਮਨਿ ਬਸੈ ਸੁ ਹੋਤ ਨਿਧਾਨ ॥
jis man basai so hot niDhaan.
Yule ambaye akilini mwake mnaishi Naam anakuwa hazina ya fadhila.
ਸਰਬ ਇਛਾ ਤਾ ਕੀ ਪੂਰਨ ਹੋਇ ॥
sarab ichhaa taa kee pooran ho-ay.
Hamu zake zote zinatimizwa,
ਪ੍ਰਧਾਨ ਪੁਰਖੁ ਪ੍ਰਗਟੁ ਸਭ ਲੋਇ ॥
parDhaan purakh pargat sabh lo-ay.
Na anakuwa maarufu duniani kote kama mtu mkuu.
ਸਭ ਤੇ ਊਚ ਪਾਏ ਅਸਥਾਨੁ ॥
sabh tay ooch paa-ay asthaan.
Yeye anapokea hali ya kiroho iliyoinuliwa zaidi.
ਬਹੁਰਿ ਨ ਹੋਵੈ ਆਵਨ ਜਾਨੁ ॥
bahur na hovai aavan jaan.
Yeye hapitii mizunguko ya kuzaliwa na kufa.
ਹਰਿ ਧਨੁ ਖਾਟਿ ਚਲੈ ਜਨੁ ਸੋਇ ॥
har Dhan khaat chalai jan so-ay.
Huyo anaondoka duniani baada ya kukusanya utajiri wa Jina la Mungu,
ਨਾਨਕ ਜਿਸਹਿ ਪਰਾਪਤਿ ਹੋਇ ॥੫॥
nanak jisahi paraapat ho-ay. ||5||
Ee Nanak, yule ambaye amebarikiwa na Mungu kwa tuzo hili.
ਖੇਮ ਸਾਂਤਿ ਰਿਧਿ ਨਵ ਨਿਧਿ ॥
khaym saaNt riDh nav niDh.
Amani ya milele, utulivu, nguvu zote za kufanya miujiza na hazina tisa za utajiri wa kidunia,
ਬੁਧਿ ਗਿਆਨੁ ਸਰਬ ਤਹ ਸਿਧਿ ॥
buDh gi-aan sarab tah siDh.
hekima, maarifa na nguvu zisizo za kawaida humjia mtu huyo (anayetafakari kuhusu Jina la Mungu).
ਬਿਦਿਆ ਤਪੁ ਜੋਗੁ ਪ੍ਰਭ ਧਿਆਨੁ ॥
bidi-aa tap jog parabh Dhi-aan.
maarifa, toba, Yoga na kumtafakari Mungu;