Page 12
ਤੂ ਆਪੇ ਕਰਤਾ ਤੇਰਾ ਕੀਆ ਸਭੁ ਹੋਇ ॥
too aapay kartaa tayraa kee-aa sabh ho-ay.
Wewe mwenyewe ndiye Muumba. Kila kitu kinachotendeka ni kwa sababu yako.
ਤੁਧੁ ਬਿਨੁ ਦੂਜਾ ਅਵਰੁ ਨ ਕੋਇ ॥
tuDh bin doojaa avar na ko-ay.
Hakuna mwingine ila Wewe.
ਤੂ ਕਰਿ ਕਰਿ ਵੇਖਹਿ ਜਾਣਹਿ ਸੋਇ ॥
too kar kar vaykheh jaaneh so-ay.
Unaumba ulimwengu mzima, unauchunga na unaulewa. Unafahamu mahitaji ya kila mtu.
ਜਨ ਨਾਨਕ ਗੁਰਮੁਖਿ ਪਰਗਟੁ ਹੋਇ ॥੪॥੨॥
jan naanak gurmukh pargat ho-ay. ||4||2||
Ee Nanak, Mungu amefunuliwa ndani mwa wale wanaoishi kulingana na mafundisho ya Guru.
ਆਸਾ ਮਹਲਾ ੧ ॥
aasaa mehlaa 1.
Raag Aasaa, na Guru wa kwanza:
ਤਿਤੁ ਸਰਵਰੜੈ ਭਈਲੇ ਨਿਵਾਸਾ ਪਾਣੀ ਪਾਵਕੁ ਤਿਨਹਿ ਕੀਆ ॥
tit saravrarhai bha-eelay nivaasaa paanee paavak tineh kee-aa.
Sisi binadamu tunaishi katika bwawa-dunia. Badala ya maji, Mungu amejaza bwawa hili na moto wa hamu ya miliki za kidunia.
ਪੰਕਜੁ ਮੋਹ ਪਗੁ ਨਹੀ ਚਾਲੈ ਹਮ ਦੇਖਾ ਤਹ ਡੂਬੀਅਲੇ ॥੧॥
pankaj moh pag nahee chaalai ham daykhaa tah doobee-alay. ||1||
Katika bwawa hili watu wamekwama katika tope nzito la viambatanisho vya kihisia na wanazama humo (hawawezi kufanya jitihada yoyote ya kujiendeleza kiroho).
ਮਨ ਏਕੁ ਨ ਚੇਤਸਿ ਮੂੜ ਮਨਾ ॥
man ayk na chaytas moorh manaa.
Ee akili yangu mpumbavu, humkumbuki Mungu Mmoja Mwenyezi.
ਹਰਿ ਬਿਸਰਤ ਤੇਰੇ ਗੁਣ ਗਲਿਆ ॥੧॥ ਰਹਾਉ ॥
har bisrat tayray gun gali-aa. ||1|| rahaa-o.
Unapoendelea kumsahau Mungu, fadhila zako zinapotea.
ਨਾ ਹਉ ਜਤੀ ਸਤੀ ਨਹੀ ਪੜਿਆ ਮੂਰਖ ਮੁਗਧਾ ਜਨਮੁ ਭਇਆ ॥
naa ha-o jatee satee nahee parhi-aa moorakh mugDhaa janam bha-i-aa.
Ee Mungu, mimi si yogi, wala mtakatifu, hata sijaelimika na nimekuwa nikiishi kama mpumbavu(nisiweze kujiokoa kutoka kwa dhambi hatari)
ਪ੍ਰਣਵਤਿ ਨਾਨਕ ਤਿਨ ਕੀ ਸਰਣਾ ਜਿਨ ਤੂ ਨਾਹੀ ਵੀਸਰਿਆ ॥੨॥੩॥
paranvat naanak tin kee sarnaa jin too naahee veesri-aa. ||2||3||
Nanak anaomba, Ee Mungu, niweke katika kimbilio la wafuasi wa Guru ambao hawajawahi kukuacha.
ਆਸਾ ਮਹਲਾ ੫ ॥
aasaa mehlaa 5.
Raag Aasaa, na Guru wa tano:
ਭਈ ਪਰਾਪਤਿ ਮਾਨੁਖ ਦੇਹੁਰੀਆ ॥
bha-ee paraapat maanukh dayhuree-aa.
Umebarikiwa na mwili mzuri wa kibinadamu.
ਗੋਬਿੰਦ ਮਿਲਣ ਕੀ ਇਹ ਤੇਰੀ ਬਰੀਆ ॥
gobind milan kee ih tayree baree-aa.
Hii ndio fursa yako ya pekee ya kugundua na kuungana na Mungu.
ਅਵਰਿ ਕਾਜ ਤੇਰੈ ਕਿਤੈ ਨ ਕਾਮ ॥
avar kaaj tayrai kitai na kaam.
Kazi zote nyingine (kupata utajiri na mamlaka ya kidunia) hazina faida kwako.
ਮਿਲੁ ਸਾਧਸੰਗਤਿ ਭਜੁ ਕੇਵਲ ਨਾਮ ॥੧॥
mil saaDhsangat bhaj kayval naam. ||1||
Hivyo basi, jiunge na ushirika mtakatifu na utafakari tu kuhusu jina lake kwa upendo na kujitolea.
ਸਰੰਜਾਮਿ ਲਾਗੁ ਭਵਜਲ ਤਰਨ ਕੈ ॥
saraNjaam laag bhavjal taran kai.
Fanya kila jitihada kuvuka bahari-dunia hii ya dhambi inayoogofya.
ਜਨਮੁ ਬ੍ਰਿਥਾ ਜਾਤ ਰੰਗਿ ਮਾਇਆ ਕੈ ॥੧॥ ਰਹਾਉ ॥
janam baritha jaat rang maa-i-aa kai. ||1|| rahaa-o.
Unaharibu maisha yako bure katika upendo wa utajiri na mamlaka ya kidunia.
ਜਪੁ ਤਪੁ ਸੰਜਮੁ ਧਰਮੁ ਨ ਕਮਾਇਆ ॥
jap tap sanjam Dharam na kamaa-i-aa.
Hujatenda utafakari, nidhamu ya kibinafsi, kujizuia na kuishi kuzuri.
ਸੇਵਾ ਸਾਧ ਨ ਜਾਨਿਆ ਹਰਿ ਰਾਇਆ ॥
sayvaa saaDh na jaani-aa har raa-i-aa.
Hujafuata mafundisho ya Guru, wala kumkumbuka Mungu.
ਕਹੁ ਨਾਨਕ ਹਮ ਨੀਚ ਕਰੰਮਾ ॥
kaho naanak ham neech karammaa.
Ee Mungu, sisi (binadamu) ni viumbe wa vitendo duni, asema Nanak.
ਸਰਣਿ ਪਰੇ ਕੀ ਰਾਖਹੁ ਸਰਮਾ ॥੨॥੪॥
saran paray kee raakho sarmaa. ||2||4||
Tunatafuta ulinzi wako, tafadhali hifadhi heshima yetu
ਸੋਹਿਲਾ ਰਾਗੁ ਗਉੜੀ ਦੀਪਕੀ ਮਹਲਾ ੧
sohila raag ga-orhee deepkee mehlaa 1
Sohilaa ~ Wimbo wa Kusifu. Raag Gauree Deepkee, na Guru wa kwanza:
ੴ ਸਤਿਗੁਰ ਪ੍ਰਸਾਦਿ ॥
ik-oNkaar satgur parsaad.
Mungu Mmoja Mkuu wa milele na wa kipekee. Anayegunduliwa kwa neema ya Guru wa kweli:
ਜੈ ਘਰਿ ਕੀਰਤਿ ਆਖੀਐ ਕਰਤੇ ਕਾ ਹੋਇ ਬੀਚਾਰੋ ॥
jai ghar keerat aakhee-ai kartay kaa ho-ay beechaaro.
Katika ushirika mtakatifu, wakati sifa za Mungu zinakaririwa na fadhila zake kutafakariwa,
ਤਿਤੁ ਘਰਿ ਗਾਵਹੁ ਸੋਹਿਲਾ ਸਿਵਰਿਹੁ ਸਿਰਜਣਹਾਰੋ ॥੧॥
tit ghar gaavhu sohilaa sivrihu sirjanhaaro. ||1||
Ee roho yangu, wewe pia enenda katika mkusanyiko huo mtakatifu na uimbe Sohila (wimbo wa sifa zake) na utafakari kuhusu Muumba kwa upendo na kujitolea.
ਤੁਮ ਗਾਵਹੁ ਮੇਰੇ ਨਿਰਭਉ ਕਾ ਸੋਹਿਲਾ ॥
tum gaavhu mayray nirbha-o kaa sohilaa.
Rafiki zangu wa dhati, imbeni Sohila (wimbo wa sifa zake) ya Mungu wangu asiye na woga.
ਹਉ ਵਾਰੀ ਜਿਤੁ ਸੋਹਿਲੈ ਸਦਾ ਸੁਖੁ ਹੋਇ ॥੧॥ ਰਹਾਉ ॥
ha-o vaaree jit sohilai sadaa sukh ho-ay. ||1|| rahaa-o.
Najiweka wakfu kwa wimbo huo wa sifa zake unaoleta amani ya milele.
ਨਿਤ ਨਿਤ ਜੀਅੜੇ ਸਮਾਲੀਅਨਿ ਦੇਖੈਗਾ ਦੇਵਣਹਾਰੁ ॥
nit nit jee-arhay samaalee-an daykhaigaa dayvanhaar.
Mfadhili mkuu, ambaye amekuwa akichunga uumbaji wake siku baada ya siku, pia atashughulikia mahitaji yako.
ਤੇਰੇ ਦਾਨੈ ਕੀਮਤਿ ਨਾ ਪਵੈ ਤਿਸੁ ਦਾਤੇ ਕਵਣੁ ਸੁਮਾਰੁ ॥੨॥
tayray daanai keemat naa pavai tis daatay kavan sumaar. ||2||
Ee binadamu, wakati huwezi hata kutathmini thamana ya zawadi zake; basi utawezaje kutathmini thamani ya Mfadhili huyo? Yeye hana mwisho.
ਸੰਬਤਿ ਸਾਹਾ ਲਿਖਿਆ ਮਿਲਿ ਕਰਿ ਪਾਵਹੁ ਤੇਲੁ ॥
sambat saahaa likhi-aa mil kar paavhu tayl.
Wakati wa kuondoka kwangu duniani humu uliamuliawa tokea mwanzo. Enyi rafiki zangu, nivisheni mavazi ya kuondoka kwenda kwa nyumba ya Bwana wangu.
ਦੇਹੁ ਸਜਣ ਅਸੀਸੜੀਆ ਜਿਉ ਹੋਵੈ ਸਾਹਿਬ ਸਿਉ ਮੇਲੁ ॥੩॥
dayh sajan aseesrhee-aa ji-o hovai saahib si-o mayl. ||3||
Enyi rafiki zangu, tafadhali nipeeni baraka zenu, ndiposa niweze kuungana na Bwana wangu.
ਘਰਿ ਘਰਿ ਏਹੋ ਪਾਹੁਚਾ ਸਦੜੇ ਨਿਤ ਪਵੰਨਿ ॥
ghar ghar ayho paahuchaa sad-rhay nit pavann.
Taarifa kuhusu tarehe na wakati wa kuondoka kutoka dunia hii inapelekwa nyumba baada ya nyumba, na kila siku watu wanaitwa.
ਸਦਣਹਾਰਾ ਸਿਮਰੀਐ ਨਾਨਕ ਸੇ ਦਿਹ ਆਵੰਨਿ ॥੪॥੧॥
sadanhaaraa simree-ai naanak say dih aavann. ||4||1||
Ee Nanak, siku hio yetu inakaribia zaidi, basi mkumbuke Mungu, yule anayetuita sote, kwa kujitolea kwa upendo.
ਰਾਗੁ ਆਸਾ ਮਹਲਾ ੧ ॥
raag aasaa mehlaa 1.
Raag Aasaa, na Guru wa kwanza:
ਛਿਅ ਘਰ ਛਿਅ ਗੁਰ ਛਿਅ ਉਪਦੇਸ ॥
chhi-a ghar chhi-a gur chhi-a updays.
Kuna Shastra sita au maandishi, na waandishi wake au Guru ni sita, na sehemu sita za mafundisho.
ਗੁਰੁ ਗੁਰੁ ਏਕੋ ਵੇਸ ਅਨੇਕ ॥੧॥
gur gur ayko vays anayk. ||1||
Lakini Guru Mkuu wa wote ni Mungu mwenyewe katika miundo isiyohesabika.
ਬਾਬਾ ਜੈ ਘਰਿ ਕਰਤੇ ਕੀਰਤਿ ਹੋਇ ॥
baabaa jai ghar kartay keerat ho-ay.
Ee Baba, baki mahala hapo ama penye ushirika mtakatifu ambako sifa za Muumba zinaimbwa.
ਸੋ ਘਰੁ ਰਾਖੁ ਵਡਾਈ ਤੋਇ ॥੧॥ ਰਹਾਉ ॥
so ghar raakh vadaa-ee to-ay. ||1|| rahaa-o.
Na uweke urafiki wa watu wanaompenda Mungu. Kwa njia hii utapokea heshima katika mahakama ya Mungu.
ਵਿਸੁਏ ਚਸਿਆ ਘੜੀਆ ਪਹਰਾ ਥਿਤੀ ਵਾਰੀ ਮਾਹੁ ਹੋਆ ॥
visu-ay chasi-aa gharhee-aa pahraa thitee vaaree maahu ho-aa.
kuna sekunde nyingi, dakika, saa, siku, wiki na miezi,
ਸੂਰਜੁ ਏਕੋ ਰੁਤਿ ਅਨੇਕ ॥
sooraj ayko rut anayk,
Na misimu tofauti kwenye mwaka. Lakini yote yanaasilia kutoka chanzo kimoja, ambayo ni jua moja. Ee Nanak, sawia kuna maonyesho yasiyohesabika ya Muumba lakini Yeye ni Mmoja tu.
ਨਾਨਕ ਕਰਤੇ ਕੇ ਕੇਤੇ ਵੇਸ ॥੨॥੨॥
Nanak kartay kay kaytay vays. ||2||2||